Tuesday, August 12, 2014

MAJAMBAZI YAUWA MUME NA MKE NA KUJERUHI MTOTO




Watu wanne wanaodhaniwa kuwa ni majambazi wamevamiana kuwaua mume na mke na kumjeruhi mtoto mchanga mwenye umri wa miezi 4 aliyeachwa na mama yake aliyeuliwa katika tukio lililotokea kijiji cha Murvyagira wilayani Ngara mkoani Kagera Ijumaa ya Agost 08,2014.

Kwa mujibu wa mtoto wa marehemu amesema majambazi hao walivamia nyumbani kwao majira ya saa 3 usiku ambapo walitumia panga na jembe kuwaua baba na mama yake na kisha kuwapora Maharage gunia moja, Radio, Gunia la Karanga, Mabati na Fedha vitu ambavyo hadi sasa thamani yake haijajulikana, huku wahalifu hao wakitokomea kusikojulikana.
Aidha baadhi ya wananchi walioongea na Blog hii, wameomba juhudi ya kuimarishwa hali ya usalama na ulinzi wilayani Ngara izidishwe hasa wakati huu ambako matukio ya mauaji yamezidi kujitokeza.
Mwili wa mwanaume ukiwa eneo la tukio baada ya kuuawa kwa kukatwa Mapanga na watu wanaodhaniwa kuwa ni Majambazi.

Mwili wa mwanamke ukiwa eneo la tukio baada ya kuuawa na majambazi hao. Mama huyo ameacha Mtoto mchanga mwenye umri wa miezi 4 aliyejeruhiwa na watu hao wanaodhaniwa ni majambazi.

No comments:

Post a Comment