Wednesday, August 13, 2014

NDOA YA MSANII LADY JAYDEE, GARDNER YADAIWA KUVUNJIKA!



Ndoa ya mwanamuziki Judith Wambura maarufu Lady Jaydee na mtangazaji mashuhuri wa radio Gardner G. Habash inasemekana imevunjika huku Gardner akihama Kimara alikokuwa akiishi na mkewe na kuhamia kwa mmoja wa ndugu zake wa karibu sana.
Chanzo cha kuvunjika ndoa hiyo bado hakijajulikana moja moja kwa moja ila wawili hao wamekuwa katika migogoro kwa muda sasa. Hii inaeelezwa kwamba siyo mara ya kwanza kutengana, lakini safari hii mambo yanaonekana kuwa magumu zaidi. 
Katika ukurasa wake wa Instgram, Jaydee ameandika: "Walking Away From Troubles" ambapo uchunguzi unaonyesha kwamba mambo si sawa hata kidogo.

Gardner kabla ya kumuoa Jide alikuwa tayari na mke halali wa ndoa na mtoto mmoja.

No comments:

Post a Comment