Tuesday, October 7, 2014

MOYO WA BINADAMU NA UTUMBO WAPATIKANA KATIKA OFISI YA MKUU WA SHULE IPELO. RUNGWE



Wananchi  wa kijiji cha  Ipelo    kata ya  kandete  wilayani rungwe  mkoani mbeya wamelazika kujichangisha  fedha kwa  lengo la kumtafuta mganga wa  kienyeji  baada  ya watoto wao kufariki   dunia kila   mda wa miezi {3}  katika  mazingra  ya  kutatanisha.

 
    Wakizungumza  na kipindi hiki wakati wa   maandamano ya  utoaji  wa  madawa  katika shule  ya  masingi   Ipelo  wananchi   hao wamesema hatua  hiyo imekuja kufuatia  vifo  vya ajabu kujitokeza  kijiji hapo  kwa watoto  wao ambao wamekuwa wakifariki kila  baada ya  miezi mtatu   na  wote  kutokomea mahali pasipo fahamika.baada ya mganga huyo kutoa vitu vya ajabu katika shule hiyo ambapo alitoa  utumbo wa binadamu ndani ya  Rambo pamoja na  moyo wa ngombe ndani ya kichupa ukiwa unahema.        Majabu.
 Hata  hivyo  imeelezwa  kuwa  mpaka sasa  watoto  wanne  walifariki  dunia  katika  mazingira  ya  kutatanisha  na kwamba  hali  hiyo  huwa  inajitokeza kwa wanafunzi  wa  darasa  la nne ambao  mpaka sasa  wamegoma kwenda  shule wakiogopa   vifo hivyo.
Aidha wakazi wa kijiji hicho wameomba msaada kwa serikali  na  watumishi wa mungu  kwa  ujumla kuwasaidia janga hilo ambalo  limeonekana kuwa  kelo  kwa     kwao.
  Sambamba na hayo  ikumbukukwe  kuwa   vitu  hivyo  viliweza  kutolewa  na mganga  huyo   vikiwa   vimefukiwa na   mtu au watu katika  ofisi ya  mkuu  wa shule  na  vikisadikiwa kuwa ndiyo chanzo  cha matatizo   hayo.
 Kwa  upande wa  viongozi wa  mitaa  hiyo  wamesema  hawawezi kuzungumza chochote  juu ya suala hilo  kutokana  na kwamba  serikali haiamiini  masuala ya  kishirikina  na kwamba mganga huyo ameitwa  na wananchi  husika  bila  wao kushirikishwa chochote.















No comments:

Post a Comment