Monday, November 24, 2014

MZEE WA MIAKA 75 AMPA MIMBA BINTI WA MIAKA 13


Matukio ya mimba za utotoni yamekuwa yakijitokeza kila kukicha yakiwa na sura tofauti, mengi yametajwa kuharibu maisha na kupoteza ndoto za wasichana wengi.

Kutoka Nigeria Mzee mwenye umri wa miaka 75 anashikiliwa na Jeshi la Polisi kwa kosa la kumpa ujauzito mwanafunzi mwenye umri wa miaka 13.Mzee huyo Pa Alabi ambaye ni fundi seremala aliombwa na binti huyo kumtengenezea kiboksi cha kuhifadhia pesa zake, baada ya kumpa kiboksi hicho akaanza kumtongoza na kujenga ukaribu nae hadi binti akakubali. 
“..Siku yenyewe nilimwelezea hisia zangu na akaahidi kulifikiria suala hilo na baadae akakubali, tulikutana kimwili pale nilipomuomba na tulikuwa tukiheshimiana, ghafla akaacha kuja kwangu baada ya siku tano baada ya ile siku ya kwanza tulipokutana kimwili. Siku moja akaja na kuniambia Bibi yake alimwambia ni mjamzito ndipo alipoacha kuja kwangu na sikumuona tena hadi Polisi walipokuja kunikamata..– Pa Alabi. 
Siku ya kwanza msichana huyo kukutana na Alabi alimpatia hela Naira 200 na kumnunulia simu ya mkononi yenye thamani ya Naira 150 pesa za Nigeria na baada ya kukamatwa na kuhojiwa alijitetea kuwa hakujua kama ni kosa kukutana kimwili na binti huyo mdogo na kueleza kuwa lengo lake ilikuwa ni kumuoa na kumtunza yeye na mtoto wake.

No comments:

Post a Comment