Friday, November 21, 2014

WABUNGE WACHARUKA KASHFA AKAUNTI YA TEGETA-ESCROW

Hawa ndio wabunge waliofunguka wakitaka sakata hilo lijadiliwe bungeni
Naibu spika wa bunge Job Dungai, yeye ndiye kashikilia rungu, Ripoti " ijadiliwe au la"
Mbunge wa Kigoma Kaskazini (CHADEMA), Ambaye pia ni mwenyekiti wa kamati ya bunge ya hesabu za serikali, (PAC), Zitto Kabwe. Taarifa ya CAG kuhusu akaunti nya Tegeta Escrow, iko mikononi mwake
Mnadhimu mkuu wa kambi ya upinzani bungeni, Tundu Lissu, (CHADEMA),akizunghumza bungeni mjini Dodoma jana, wakati lile sakata la IPTL, linalogubigwa na akauti iliyojichukulia umaarufu TEGETA ESCROW, lilipoibuka bungen i wakati wa kipindi cha maswali ya papo kwa hapo kwa waziri mkuu. Wabunge wanataka "ngoma" ijadiliwe bungeni, licha ya kashfa hiyo kuwa tayari mahakama kuu ya Tanzania
Mbunge wa Kigoma Kusini, (NCCR-Mageuzi), David Kafulila, huyu ndiye aliyeibua kashfa ya akaunti ya Tegeta-Escrow
Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki na mbunge wa Urambo, (CCM), Samwel Sitta
Mbunge wa Iringa mjini, (CHADEMA), Mchungaji Peter Msigwa
Mbunge wa kuteuliwa na Rais, ambaye pia ni Mwenyekiti wa NCCR-M,ageuzi, James Mbatia
Mbunge kijana, Esther Bulaya, (CCM)
Mbunge wa Longido,(CCM), Lekule Laizer,
Mbunge wa Kasulu mjini (NCCR-Mageuzi), Moses Machali, ndiye aliyemchokoza Waziri mkuu kuhusu ripoti hiyo kujadiliwa bungeni
Waziri Mkuu Mizengo Pinda, "Punguzeni jazba", akiwasihi wabunge kuwa serikali iko makini na inasubiri kwa hamu taarifa hiyo ili kila mtu hata yeye akibainika abebe msalaba wake, lakini akatahadharisha kuhusu umuhimu wa kuheshimu mihimili ya dola ikiwemo mahakama
Mbunge wa Kahama (CCM), James Lembeli

No comments:

Post a Comment