Monday, December 1, 2014

WANANCHI WAASWA KUPANDA MICHE YA MATUNDA ILIYOBORESHWA





Kutokana na elimu ya kilimo kutolewa katika Nyanja mbalimbali watanzania wameonekana kuwa na mwamko wa kutumia mbegu na miche ya kisasa katika kilimo chao.

Hayo yamesemwa na msemaji wa BRIDEBABLE CONSULTANT LTD ya jijini Dar Mr Michael Lameck ambopo amesema wananchi wengi wamekuwa na muamko wa  kutumia mbegu bora katika kilimo, hivyo kuwaasa pia kutumia miche ya matunda iliyoboreshwa kiteknolojia zaidi.

msemaji huyo amesema kuwa upandaji wa miche ya matunda iliyo zalishwa kwa kutumia bioteknolojia ya uzalishaji kwa njia ya chupa na uzalishaji kwa kutumia vikonyo huleta tija katika kilimo cha matunda. kutokana na  watu kuwa na mwamko wa kula matunda pamoja na juisi za asili hivyo kumekuwa na uhitaji mkubwa wa matunda mijini hivyo amewaasa vijana kuchangangamkia tenda hii kwa kujikita katika kilimo

Ili kuepuka uagizaji wa matunda kutoka nje ya nchi kama ilivyo tunda la tufaa ambalo huletwa nchini kutoka nchi ya Afrika ya kusini amewataka vijana kujiajiri wenyewe katika kilimo kwa kulima matunda ambayo hayahitaji mkulima kuwa shambani wakati wote na hulimwa hata nyumbani kwa faida ya familia.

Bwana Michael akionyesha jinsi miche miwili ilivyounganishwa ili kupata mche mmoja 

Bridebable Consultant ni kampuni iliyoko jijini Dar inayouza miche bora ya matunda kwa wakulima nchini na nje ya nchi kulingana na mahitaji ya mkulima mwenyewe

Miche hii ambayo imeboreshwa na kituo cha utafiti na kilimo SUA ni miche ambayo hukua haraka na kuzaa matunda bora na kwa wingi. Miti hii ya matunda ni miti ambayo huchukua mda mfupi kuanza kuzaa matunda hivyo haimfanyi mkulima kusubiri mda mrefu kupata manufaa yake.

Bwana Michael alisema miche ya matunda ambayo inapendwa sana na watu wengi wa jiji la Dar ni pamoja embe aina ya Red Indian, Apple Mango, Alphonso, Cant, embe sindano na alizeti/dodo, pia kuna  Mapera, Minazi ya mda mfupi pamoja na machenza.

kilimo cha miti ya matunda yanaweza kupandwa nyumbani na kumnufaisha mtu kwa kula matunda na kutumia miti hiyo kama kivuli nyakati za jua kali, pia miti hupendezesha mazingira iwapo itapandwa katika utaratibu mzuri


 Baadhi ya miche inayouzwa na Bridebable

 Hata hivyo alisema kampuni yake inauza aina zote za miti japo kuwa kuna aina ya miti huuzwa kwa oda maalumu. hivyo yeyote mwenye mahitaji ya miti nyumbani au shambani kwake wasiliana nao kwa kuwapigia

+255 712545052, +255 784 647775 au waandikie  upambamichael@gmail.com


No comments:

Post a Comment