Thursday, September 11, 2014
IPTL YAMDAI ZITTO KABWE FIDIA YA SH. BILIONI 500
Kampuni ya kufua umeme ya Independent Power Tanzania Limited (IPTL), imefungua kesi ya madai katika Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam, wakimtaka Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe awalipe fidia ya Sh bilioni 500 kutokana na kutoa kashfa dhidi yao.
IPTL, Kampuni ya Pan Africa Power Solutions Tanzania Limited (PAP) na Mwenyekiti Mtendaji wa makampuni hayo mawili, Harbinder Seth wamefungua kesi dhidi ya Zitto, Mhariri wa gazeti la Raia Mwema, Kampuni ya Raia Mwema na Kampuni ya Flint Graphics.
Washitakiwa wengine wameshitakiwa kwasababu makala yenye maneno ya kashfa na kuwachafua, iliyochapishwa Agosti 13 mwaka huu katika ukurasa wa 7 na 14 wa gazeti lao, ikiwa na kichwa cha habari cha “Fedha za IPTL ni Mali ya Umma” na Kampuni ya Flint Graphics kwa kuchapisha gazeti hilo.
Aidha, wanaiomba Mahakama iamuru makala hayo, yalikuwa ya upotoshaji na kuwachafua kwa kudhamiria, pia wadaiwa waombe radhi kwa kuchapisha habari ya kuomba msamaha kwenye kurasa za mbele katika matoleo mawili mfululizo ya gazeti hilo.
Wadaiwa hao waliiomba Mahakama, itoe zuio kwa wadaiwa, watumishi wao, wafanyakazi, washirika, wawakilishi au watu wengine wanaofanya kazi chini ya wadaiwa, kuchapisha au kuandika makala yoyote ya kuwachafua.
UKAWA WAMVAA RAIS KIKWETE TENA
SIKU moja kupita baada ya Rais Jakaya Kikwete kufikia Maazimio na Umoja
wa Kutetea Katiba ya Wananchi UKAWA kulisitisha bunge Maalum la katiba
na kupisha Uchaguzi mkuu wa Mwaka 2015 ili kutoa mwanya wa kuifanyia
marekebisho ya 15 ya katiba iliyopo ya Mwaka 1977,
Nao Umoja huo wa kutetea Katiba ya Wananchi UKAWA umeibuka na
kumvaa Rais Jakaya Kikwete na kumtaka asitishe Bunge hilo mara moja na
kuacha mpango wake wa kulisitisha Bunge hilo Octoba 4,kwani kufanya
hivyo ni kupoteza pesa za Watanzania bure kutokana Vikao hivyo
vinavyoendelea haviwezi kuleta katiba bali vinaendelea kuteketeza pesa
za Wananchi,
Hayo yamesemwa leo jijini Dar Es Salaam na Viongozi mbalimbali wa
kisiasa wanaunda Umoja wa Kutetea Katiba ya Wananchi UKAWA,wakati wa
Mkutano na Waandishi Habari, mkutano huo wenye Lengo la kujadili
maazimio kati ya viongozi wa Kituo cha Demokrasia Tanzania (TCD),na Rais Jakaya kikwete uliomalizika Juzi Ikulu ndogo mjini Dodoma.
Ambapo naye katibu Mkuu wa Chama Cha Demokrasia na Mandeleo
Chadema Dk Wilbroad Slaa amesema anamshangaa sana Rais Jakaya Kikwete
kwa kutokuwa na huruma kwa watanzania kwa kuzidi kuliruhusu Bunge hilo
kuendelea hadi Oktoba 4 mwaka
huu, kwani huko ni kupoteza pesa za watanzania kutokana na yeye Rais
Kikwete wakati wa mkutano na Vyama vya hivyo vya Kisiasa alikibuliana
nao kwamba Mwenendo wa Bunge hilo hauwezi kuleta Katiba Mpya,
“Mimi namshangaa jinsi Rais Kikwete anavyokubalia pesa za Watanzania
zipotee bure kiasi hichi pasipo kuwa na Sababu maana leo hii mpaka
octoba 4 ni siku ishirini na ukipiga hesabu za Wajumbe wote waliokuwa
Bungeni kwenye Vikao vya Bunge garama yake ya posho ni zaidi ya Bilioni
3.5 hurafu yeye mwenyewe Kikwete anakubali wazi katiba haitopatikana
sasa, huku ni kuchezea pesa za wananchi kabisa maana ukweli huko wazi
kabisa ndio maana tunamtaka sisi UKAWA alisitishe sasa bunge hilo ili
fedha hizo ziende katika mambo mengine yenye tija”alisema Dokta Slaa,
Dokta Slaa alizidi kusema anamshangaa Rais Jakaya Kikwete kwa kutokuwa
na huruma za watanzania kwani anakubalina na watu mia sita kutoka kwenye
bunge hilo laa Bunge la katiba na kuwapuuza watanzania Zaidi ya
Milioni 40 ambao hata mlo moja kwa siku ni kazi.
“Huyo ni Rais gani huyo ambaye anashindwa hata kuwaonea huruma
watazania wanaoteseka tena hata kula mlo moja kwa siku ni kazi,yeye
anakubaliana na wajumbe mia sita kuteketeza pesa za Wananchi,hivi kweli
ndio kiongozi huyu,kwasababu kiongozi makini ni yule anayeangalia Fedha
za Chache kwa ajili ya manufaa kwa wananchi wake”alizidi kusema Dokta
Slaa.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa Chama cha NCCR mageuzi James Mbatia
alisema wao Ukawa wamepokea kwa moyo wote maamuzi waliyofikia ya
kuifanyia marekebisho ya katiba iliyopo na kusema Bunge la katiba
litakapohalishwa basi wakubaliane kamaandishi ili Rais ajaye basi aendelee na mchakato huu asiupuuze,
“Sisi ukawa tunakubalina na kwa moyo wate maanuzi tulitofikia katika
mkutano na Rais Kikwete,na tunasema wazi tumekubaliana kuhailisha
mchakato huu basi tunataka tukubaliane kimaandishi kabisa ili Rais ajaye
baada ya Uchaguzi wa Mwaka 2015 aendelee na mchakato huu atutaki kabisa
kusikia eti Rais anayekuja ahamue kwa maamuzi yake hatutati kusikia
ujinga huo”alisema Mbatia
Mbatia ambaye naye ni Mjumbe wa Bunge hilo Maalum la katiba aliongeza
kusema wao Ukawa wamefikia uamuzi kwamba endapo Bunge hilo la katiba
litakapoendelea baada ya uchaguzi mkuu hawatakubali kuongozwa na
mwenyekiti wa sasa ambaye anaongoza Samwel Sitta na kuzidi kusema
Mwenyekiti huyo hana sifa ya kuliongoza bunge hilo kutokana na
kuendesha siasa za chuki na ubaguzi.
Vilevile naye Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi CUF Profesa
Ibrahimu Lipumba alisema wanamuomba Mkaguzi mkuu wa Hesabu za Serikali
kulikagua Bunge hilo la Katiba kwa madai bunge hilo lilitawaliwa na
Ufisadi wa kutisha kutokana mipango yake hiyo.
“Kiukweli namuomba Mkaguzi Mkuu wa Serika alifanyie ukaguzi wa
kimahesabu bunge hilo la katiba kutokana na Vikao vyake hivyo kutawaliwa
na ufisadi wa kutisha tumeona leo Jinsi kila mjumbe mmoja kwa siku
ametengewa bajeti ya chai ya shilingi Eflu kumi kwa siku tena chai ya
asubuhi na jioni na hata vipaza sauti pia, vyote hivi ni matokeo ya
Ufisadi ndio maana tunamtaka alifanyie ukaguzi wa kimahesabu”alisema
profesa Lipumba.
Kuhusu kama Endapo Rais Jakaya asipofanyia merekebisho katiba iliyopo?
Mwenyekiti
wa Chama cha NCCR mageuzi James Mbatia alisema endepo kama Rais Kikwete
asipofanyia marekebisho katiba iliyopo basi atakuwa amefanya usaliti
kubwa na ajue ataliweka taifa kwenye machafuko makubwa sana kwani Umoja
huo hautokubaliana na yeye.
Katika Hatua nyingene Umoja huo wa Katiba wa UKAWA umeitaka tume ya
Uchaguzi nchini ilifanyie marekebisho ya haraka Daftari la kudumu la
wapiga kura ili liweze kuwaandikisha watanzania ambao hawajapata Fursa
hiyo.
MTANZANIA APEWA CHEO BET
Kabla ya kuanza kukupa info kuhusu huyu Mtanzania nataka nikukumbushe headlines chache za Watanzania walioingia kwenye headlines za kimataifa hivi karibuni.
Ni CloudsTV International kufungua ofisi Kingston Jamaica ambayo itahudumia ukanda wa Caribbean, Diamond Platnumz kuchaguliwa kushiriki tuzo za MTV Europe, AzamTV kuanza kufanya kazi Uganda kwa kuhudumia mamilioni kupitia king’amuzi chake na power bank za Puku zinazomilikiwa na Mtanzania aishie Marekani.
Sasa hivi vichwa hivyo vya habari vitaongezewa hii kubwa nyingine baada ya Mtanzania Kay Madati kuchaguliwa kuwa makamu wa Rais katika kituo kikubwa cha Television nchini Marekani BET.
Taarifa iliyoandikwa na Mtandao maarufu wa Forbes imesema amechaguliwa ‘Kay Madati as Executive Vice President and Chief Digital Officer. Madati, a Tanzanian citizen who has lived in Africa, the United Kingdom, and the United States’
Nilikua sifahamu kama Madati ambae ni raia wa Tanzania aliyeishi UK, Marekani na Afrika, aliwahi kuwa makamu wa Rais CNN Worldwide… aliwahi pia kufanya kazi na BMW Amerika kaskazini, Octagon Worldwide lakini pia amefanya kazi na Facebook.
‘Madati was most recently the Head of Entertainment and Media on the Global Marketing Solutions team at Facebook Inc‘
Sehemu ya kazi ya Madati BET itakua ni kuziongoza timu za BET kwenye maswala ya digital ‘will oversee BET Digital, the interactive arm of BET Networks whose platforms include BET.com, which encompasses entertainment, music, culture, and news; BET Mobile, which provides apps, ringtones, games and video content for wireless devices; Centric.tv, the online home for the Centric cable channel; and BET Video On Demand, one of the largest VOD services providing African-American content‘
ALIYEDAIWA KUUAWA KWA KIPIGO CHA POLISI, UKWELI WAJULIKANA
Waombolezaji wakitoa heshima za mwisho kwa marehemu, Liberatus Damiani Temu (55) anayedaiwa kufariki kiutata.
KIFO cha
mfanyabiashara aliyeshikiliwa katika Kituo cha Polisi cha Stakishari,
Ukonga jijini Dar es Salaam, Liberatus Damiani Temu (55) kilichodaiwa
kilitokana na kipigo kutoka kwa askari wa kituo hicho sasa ukweli
umejulikana.Chanzo makini kililiambia gazeti hili kuwa utata wa tukio hilo ulianzia mbali kwani Mei, mwaka huu, marehemu alimgonga na gari mtu mmoja anayefahamika kwa jina la Hamis Magoma na kujeruhiwa vibaya.
Mke wa marehemu, Naomi Liberatus (katikati) akihuzunika kwa kumpoteza mwenzake.
Baada ya kusababisha ajali hiyo,
ilidaiwa marehemu Liberatus alifuatilia masuala ya bima ili aweze
kumlipa aliyemgonga ambaye pia anatajwa kuwa mteja mzuri katika Baa ya
Meku iliyokuwa ikimilikiwa na marehemu.
Naomi Liberatus akiwa amezimia wakati wa mazishi.
Chanzo kinasema baada ya kutokea kwa ajali hiyo, hali ya Magoma iliendelea kuwa mbaya hadi Agosti 22, mwaka huu saa tano usiku marehemu alipokamatwa na kufikishwa kituoni hapo akidaiwa kumjeruhi Magoma kwenye ajali.
Padri akiiombea roho ya marehemu ya marehemu (Liberatus Damiani Temu).
Mke wa marehemu, Naomi Liberatus aliyezimia mara mbili wakati wa mazishi, alisema
mumewe ambaye kwa kipindi chote tangu apate ajali hiyo, alikuwa hafanyi
shughuli yoyote, alikataliwa kupewa dhamana kwa madai kuwa majeruhi
(Magoma) alikuwa na hali mbaya.
Mwili wa marehemu Liberatus Damiani Temu ukichukuliwa kwenye gari kwa ajili ya mazishi.
Kuhusu hatua nyingine
ilidaiwa kuwa marehemu akiwa mahabusu aligonga kichwa chake kwa nguvu
ukutani, hali iliyosababisha wenzake kupiga kelele za kuomba msaada na
kwamba baada ya askari kufika na kukuta hali ilivyo, walimkimbiza
Hospitali ya Taifa Muhimbili kwa matibabu ambako alifariki dunia.
Marehemu Liberatus Damiani Temu enzi za uhai wake.
“Watu wanasemasema tu kwamba Liberatus aliuawa na askari, si kweli. Kwa nini tumuue? Kwa kosa lipi?
Sisi tulimshikilia kwa sababu hali ya majeruhi aliyemgonga ilikuwa
mbaya, hivyo kumweka mahabusu marehemu ilikuwa kwa ajili ya usalama wake
pia.
KIJANA AUAWA AKITUHUMIWA USHIRIKINA MKOANI MBEYA
Marehemu akipakiwa kwenye gari tayari kumpeleka chumba cha kuhifadhia maiti.
Marehemu Gabriel Mwasyebule enzi za uhai wake.
Nyumba ya marehemu, Gabriel Mwasyebule anayotuhumiwa kuijenga kwa uchawi.
Moja
ya shamba la viazi vinavyo subiriwa kuvunwa mwezi huu, shamba la
marehemu, Gabriel Mwasyebule, mashamba amabayo pia ni moja ya sababu
ambazo wananchi wa lwangwa wanamtuhumu marehemu kuwa alikuwa
anawalimisha watu kiuchawi na kuiba mazao ya mashamba mengine kiuchawi
ili shamba lake liwe na mazao mengi na mazuri.
Hii ndio stoo kuwekea mazao mbalimbali ambayo marehemu alikuwa anatumia kutunzia mazao yake.
MATUKIO
ya kujichukulia sheria mikononi bado yanazidi kuyakumba baadhi ya
maeneo mkoani Mbeya ambapo katika tukio hili kijana Gabriel Mwasyebule
miaka 39 ameuawa na wananchi wenye hasira kali wakimtuhumu kwa imani za
kishirikina.
Kamanda
wa Polisi Mkoa wa Mbeya, Ahmed Msangi, amethibitisha kutokea kwa kifo
hicho na kumtaja marehemu aliyetambulika kwa jina la Gabriel Mwandemwa
(Mwasyebule) mkazi wa kijiji cha Ikamambande (Lwangwa) Wilaya ya Rungwe
aliuawa na watu wasiofahamika kwa kukatwa na vitu vyenye ncha kali
sehemu za kichwani na kifuani.
Alisema
tukio hilo lilitokea siku ya jumapili majira ya saa tano asubuhi huko
katika Kijiji cha Ikamambande, kata ya Lwangwa, Tarafa ya Busokelo,
Wilaya ya Rungwe, mkoaniMbeya
Alisema
taarifa za awali zinadaiwa kuwa, uongozi wa kimila kijijini hapo
uliitisha kikao cha dharura ukihusisha viongozi wa vitongoji na vijiji
jirani na ndipo waliamua kumtafuta na kumlazimisha marehemu kuhudhuria
katika kikao hicho na kisha kuanza kumpiga na kupelekea kifo chake.
Alisema
marehemu alikuwa akituhumiwa kuwa ni mshirikina kijijini hapo kwa kuwa
anawaroga watoto na kuwa anajipatia mazao mengi ya mavuno ya viazi na
kujipatia pesa zilizowezesha ujenzi wa nyumba yake aliyoweka marumaru na
Gipsam pia kumiliki pikipiki moja huku akitarajia baada ya mavuno
mazuri ya mwaka huu kununua gari la kutembelea.
Tuesday, September 9, 2014
WATAWA NA MAAJUZA WABAKWA MPAKA KUFA
Maafisa wa kanisa wanasema kuwa watawa hao waliuawa na mhali mwenye akili pungwani
Watawa watatu wakongwe wamebakwa na kuuawa mjini Bunjumbura katika makazi ya watawa wanawake viungani mwa mji mkuu huo.
Sababu
ya mauaji hayo haijulikani. Polisi wanasema kuwa wamewazuilia washukiwa
wawili, kulingana na shirika la habari la Reuters.
Watawa hao walisemekana kuwa Lucia Pulici,mwenye umri wa miaka 75, Olga Raschietti, 82 na Bernadetta Boggian, 79.
Wawili kati ya waathiriwa, waliuawa Jumapili huku mwili wa mwingine wa tatu ukipatikana Jumatatu ukiwa umekatwakatwa.
Maafisa wakuu wanasema kuwa mshukiwa wa mauaji hayo, alionekana akitoroka makazi ya watawa hayo akiwa ameshika kisu mkononi
Dayosisi ya Italia ya Parma inasema kuwa watawa hao waliuawa wakati wa jaribio la wizi katika makazi yao.
Hata hivyo haijulikani kwa nini watawa hao waliuawa kwani hakuna kilichoibwa kutoka kwao.
Watawa hao wawili walikuwa wanashiriki katika kanisa katoliki la Xaverian.Kwenye
mtandao wake, dayosisi ya kikatoliki ya Parma ilisema kuwa mauaji ya
watatu hao yalifanywa na mhalifu ambaye alikuwa na matatizo ya kiakili.
Mnamo mwaka 2011,mtawa mmoja na mfanyakazi wa shirika la misaada aliuawa katika tukio la ujambazi Kaskazini ya Burundi
Burundi ni moja ya nchi masikini ambapo uchumi wake unategemea sana mapato kutokana na Chai na Kahawa zinazouzwa nje
Subscribe to:
Posts (Atom)
.jpg)






