Thursday, September 11, 2014

ALIYEDAIWA KUUAWA KWA KIPIGO CHA POLISI, UKWELI WAJULIKANA


Waombolezaji wakitoa heshima za mwisho kwa marehemu, Liberatus Damiani Temu (55) anayedaiwa kufariki kiutata.
 KIFO cha mfanyabiashara aliyeshikiliwa katika Kituo cha Polisi cha Stakishari, Ukonga jijini Dar es Salaam, Liberatus Damiani Temu (55) kilichodaiwa kilitokana na kipigo kutoka kwa askari wa kituo hicho sasa ukweli umejulikana.Chanzo makini kililiambia gazeti hili kuwa utata wa tukio hilo ulianzia mbali kwani Mei, mwaka huu, marehemu alimgonga na gari mtu mmoja anayefahamika kwa jina la Hamis Magoma na kujeruhiwa vibaya.

Mke wa marehemu, Naomi Liberatus (katikati) akihuzunika kwa kumpoteza mwenzake.
 Baada ya kusababisha ajali hiyo, ilidaiwa marehemu Liberatus alifuatilia masuala ya bima ili aweze kumlipa aliyemgonga ambaye pia anatajwa kuwa mteja mzuri katika Baa ya Meku iliyokuwa ikimilikiwa na marehemu.
Naomi Liberatus akiwa amezimia wakati wa mazishi.
Chanzo kinasema baada ya kutokea kwa ajali hiyo, hali ya Magoma iliendelea kuwa mbaya hadi Agosti 22, mwaka huu saa tano usiku marehemu alipokamatwa na kufikishwa kituoni hapo akidaiwa kumjeruhi Magoma kwenye ajali.
Padri akiiombea roho ya marehemu ya marehemu (Liberatus Damiani Temu).
Mke wa marehemu, Naomi Liberatus aliyezimia mara mbili wakati wa mazishi, alisema mumewe ambaye kwa kipindi chote tangu apate ajali hiyo, alikuwa hafanyi shughuli yoyote, alikataliwa kupewa dhamana kwa madai kuwa majeruhi (Magoma) alikuwa na hali mbaya.
Mwili wa marehemu Liberatus Damiani Temu ukichukuliwa kwenye gari kwa ajili ya mazishi.
Kuhusu hatua nyingine ilidaiwa kuwa marehemu akiwa mahabusu aligonga kichwa chake kwa nguvu ukutani, hali iliyosababisha wenzake kupiga kelele za kuomba msaada na kwamba baada ya askari kufika na kukuta hali ilivyo, walimkimbiza Hospitali ya Taifa Muhimbili kwa matibabu ambako alifariki dunia.
Marehemu Liberatus Damiani Temu enzi za uhai wake.
 “Watu wanasemasema tu kwamba Liberatus aliuawa na askari, si kweli. Kwa nini tumuue? Kwa kosa lipi? Sisi tulimshikilia kwa sababu hali ya majeruhi aliyemgonga ilikuwa mbaya, hivyo kumweka mahabusu marehemu ilikuwa kwa ajili ya usalama wake pia.

No comments:

Post a Comment