Friday, November 21, 2014

WABUNGE WARUKA UKUTA KUINGIA BUNGENI...



Ukweli ni kwamba kuna story ambayo unaweza ukasimuliwa na rafiki yako ama mtu yoyote halafu ukaona kama ni uzushi na hakuna ukweli wowote.
Pata picha pale ambapo Spika wa Bunge pamoja na Wabunge wanafungiwa geti la kuingia ndani ya Ukumbi Bunge …
Nakupa story kutoka Nigeria, Spika wa Bunge la Nchi hiyo Aminu Tambuwal amelazimika kuingia ndani ya Bunge kupitia mlango mdogo wa dharura baada ya Polisi kufunga milango ya Bunge hilo kwa sababu za kiusalama.
Spika huyo alijitambulisha kwa Maafisa Usalama hao ili wamruhusu aingie lakini hakuna aliyeonekana kujali ombi lake wala kumjibu, japo baadaye walimruhusu aingie kupitia mlango mdogo wa dharura huku wabunge wengine wakizuiwa kuingia kitendo kilichowafanya waamue maamuzi magumu ya kuingia ndani ya Bunge kwa kuruka ukuta.
Mkuu wa Jeshi la Polisi Nigeria, Suleiman Abba amesema walilazimika kuzuia mtu yeyote kuingia ndani ya jengo hilo na kuweka ulinzi wa hali ya juu baada ya kupata taarifa kwamba kuna majambazi walipanga kuvamia Bunge hilo.Polisi waliwashambulia kwa gesi ya machozi Wabunge waliokaidi amri ya kutokuingia Bungeni, Wabunge wawili walipoteza fahamu katika vurugu hizo

KUNA BIASHARA YA WASANII WA KIKE WA MUVI INAENDELEA


Jokate Mwegelo akipozi.
 Stori:  Waandishi Wetu
Imefichuka! Kwa muda mrefu kumekuwa na taarifa za chini kwa chini kwamba baadhi ya mastaa wa kike Bongo, hasa wale wa filamu ‘Bongo Movies’ huuzwa kwa wanaume, mara nyingine kwa kujua au kutojua lakini wenyewe wamekuwa wakikanusha hivyo kutoa ‘kibarua’ kwa Ijumaa kuingia mzigoni kisha kumuibua mmoja wa wahusika (kuwadi) anayerahisisha biashara hiyo haramu ya ngono.

Uchunguzi wa gazeti hili ulibaini kwamba, kuwadi huyo huwa anajua dau la kila staa hivyo anapopata mwanaume hasa mapedeshee, wafanyabiashara na baadhi ya vigogo serikalini, huwaunganisha kwa kutoa namna ya mawasiliano au kuwaunganisha moja kwa moja.

Uchunguzi huo ulibaini uwepo wa madai mazito kwamba wapo baadhi ya mastaa wa kike wa Bongo Movies ambao hugombewa na makuwadi kwa sababu wana soko kubwa.
“Jaribu kufikiri msanii haonekani location (eneo la kuigizia sinema) wala sinema aliyocheza haijulikani lakini muda mwingi utamuona anatanua kwenye viwanja vya starehe, lazima ujiongeze kwamba kipato kinatoka wapi?
 
Staa wa filamu Bongo Aunt Lulu.
“Mimi nakwambia hii Bongo Movies imebaki jina tu, sioni mwanga mbeleni kwa sababu hawa mabinti hawapo serious zaidi ya kutafutiwa wanaume,” kilidai chanzo chetu ambacho ni mfuatiliaji wa karibu wa kazi za sanaa Bongo.

Madai mazito yaliendelea kushushwa kwamba wapo wanunuaji ambao huhonga magari (bila kadi) ambapo baadaye hukamatwa kimafia na kurejeshwa kwa mhongaji.
Ikazidi kufahamika kwamba, mastaa wenye sifa ya kuhongwa magari ni wale wenye majina makubwa.
Staa wa filamu Bongo, Jacqueline Wolper Massawe.

Ilisemekana kwamba wapo mastaa wanaotajiwa dau kubwa kuanzia Sh. milioni tano na kuendelea na wapo wa chini ya hapo hadi buku hamsini (50,000).
Mpaka sasa kuna mastaa wanaowindwa na makuwadi kwa kuwa wana soko na bei zao kwenye mabano ni pamoja na Elizabeth Michael ‘Lulu’ (Mil. 5), Jokate Mwegelo (Mil. 5), Wema Isaac Sepetu (Mil. 5), Kajala Masanja (Mil. 5) na Jacqueline Wolper Massawe (Mil. 5).
 
Staa wa filamu Bongo, Jacqueline Pentzel ‘Jack Chuz’.
Wengine ni Baby Joseph Madaha (Mil. 5), Miriam Jolwa ‘Jini Kabula’ (Mil. 3), Aunty Ezekiel (Mil. 3), Jennifer Mwaipaja ‘Shumileta’ (Mil. 2) Isabela Francis ‘Vai wa Ukweli’ (Mil. 1), Lulu Mathias ‘Anti Lulu’ (Mil. 1), Jacqueline Pentzel ‘Jack Chuz’ (Mi. 1) na wengine kibao ambapo kwa sasa upepo umegeukia kwa wale wanaochipukia.
 
Katika kusaka ukweli juu ya skendo hiyo, jina la mmoja wa makuwadi hao ambaye ni mwigizaji wa kike Bongo, Lungi Maulanga (pichani) ilitajwa.
Staa wa filamu Bongo, Elizabeth Michael ‘Lulu’.
Mbali na Lungi pia alitajwa mwigizaji mmoja wa kiume wa Bongo Movies na jamaa mwingine ambaye huwa ni mdandiaji wa ishu za mastaa (majina tunayo, tutayataja tukijiridhisha kisheria).

Baada ya kutajiwa jina la Lungi, gazeti hili lilimsaka mwigizaji huyo anayedaiwa kuwauza baadhi ya mastaa hao kwa wanaume ambapo alibanwa vilivyo hadi akaanika siri nzito nyuma ya biashara hiyo kubwa isiyo na kodi.
 
Staa wa filamu Bongo, Wema Sepetu.
Mbali na kukiri kuwakuwadia mastaa hao kipindi cha nyuma kabla ya kuacha, Lungi alifunguka kwamba amekuwa akisumbuliwa na wanaume wakware wakitaka awaunganishe na mastaa ambao alidai alishafanya nao kazi hiyo muda mrefu.
MSIKIE LUNGI Ijumaa: Habari yako Lungi... Lungi: Nzuri, mmekuja kufuata nini hapa (nyumbani kwake Kinondoni, Dar)? Ijumaa: Mbona unajihami? Tumekuja kukusomea mashitaka yako! Lungi: Mashitaka gani? Siku hizi nimetulia, sijichanganyi kama zamani, kulikoni tena? Ijumaa: Hapa kuna madai mazito...
 
Staa wa filamu Bongo, Vai wa Ukweli.
Lungi: Hebu semeni kilichowaleta, kwanza siku hizi sipendi kukutana na waandishi wa habari! Ijumaa: Kuna za chinichini kwamba wewe ndiye unayewauza mastaa wa Bongo na ndiyo biashara inayokuweka mjini kwa kuwa hata location huonekani. Je, ni kweli?
Lungi: (kwa hasira) yaani mimi niwekwe mjini na mastaa? Kwani hamjui anayeniweka mjini? Au mnataka niwafukuze na panga?Ijumaa: Kwa nini unakuwa mkali Lungi? Unachotakiwa kufanya ni kutoa majibu kwa sababu kuna shosti’ako ametutajia staa uliyemuuza juzi tu!
Staa wa filamu Bongo, Aunty Ezekiel akipozi.
Lungi: (bila kujua anarekodiwa) juzi! Sikieni, nawaheshimu sana, mimi nilikuwa nikifanya biashara hiyo siku nyingi na niliacha kwa sababu hao mastaa hawana maana, wakishapata wanajisikia na kusahau walipotoka.
“Huyo aliyewaambia ana ushahidi gani kama juzi nimeshamuuza staa? Ijumaa: Oke, tuache hilo! Unakumbuka dau kubwa ulilowahi kupewa wakati unawakuwadia? Lungi: (kwa mara ya kwanza anatabasamu) nilishawahi kupata hadi Sh. milioni tatu na kima cha chini laki tano, lakini jamani mbona ni siku nyingi?
 
Staa wa filamu Bongo, Lungi Maulanga.
“Kwanza mimi sitaki hizo habari kabisa. Nimechoka kusumbuliwa na wanaume kwa ishu hizo.”Ijumaa: Hilo dau kubwa ulilipata kwa mwanaume wa Dar, mikoani au nje ya nchi?Lungi: Watu wa mikoani ndiyo wanakata mkwanja mkubwa, hapa Dar longolongo tu. Hiyo Sh. milioni tatu niliipata kwa jamaa mmoja wa Arusha.

KIJANA SANDE MREMI AFARIKI DUNIA,NDEGE ZILIGOMA KUMSAFIRISHA

Sande Jacob Mremi amefariki Siku chache baada ya kukosa usafiri wa ndege ambapo alitakiwa kwenda nje ya nchi kupata matibabu.Kituo cha ITV kiliripoti kuhusu habari za kijana huyo kuumwa na kutokana na kusumbuliwa tatizo la uzito mkubwa nakushindwa kupata Ndege ya kumsafirisha kwenda kwenye matibabu India kijana huyo amefariki Dunia.Ndugu wa kijana huyo walilalamika kutoridhishwa na baadhi ya Mashirika ya Ndege kwa kushindwa kuwasaidia kumsafirisha ndugu yao.Katika mahojiano na ITV mama wa mtu huyo amesema; “..yaani kwa kweli mashirika ya Ndege hayakuweza kutufanyia haki kwa kweli, wametunyanyasa kwa sababu tulipokuwa tunapeleka maombi tunataka kumsafirisha mtoto wetu ilikuwa wao watusaidie na kutupa maelekezo tunatakiwa tufanye nini na nini, lakini baada ya kuona tunakosa msaada ndio tukaamua kuja ITV ili watusaidie, kwa hiyo yeye mwenyewe akaanza kupata presha kwa sababu presha alikuwa hana mpaka anapanga kusafiri alikuwa hana presha nilimpima vipimo vyote alikuwa hana tatizo lolote…”

Dada wa marehemu amesema; “..Ethiopia walitusaidia kwa kweli mpaka hatua ya mwisho na Jumapili kama Mungu angemuweka hai Ethiopia wangemsafirisha, na mashirika ya Ndege mengine yalitakiwa yatuelekeze hivi, lakini sasa kutokana na ile hali mara leo kapelekwa kesho anarudishwa mdogo wangu kesho kutwa kapelekwa amerudishwa mdogo wangu, msongo wa mawazo umemkaa rohoni anashindwa kuongea maskini ya Mungu, mawazo paka yamemfanya mdogo wangu alikuwa hana presha paka presha imekuja paka mdogo wangu anafariki.
sds
Baba wa Sande amesema; “…wakatumia sheria ya pili ya kunihusisha mimi wakaniambia bwana kumbe mtu huyu ni mkubwa sana tunatakiwa tuvunje viti tumbebe, nikawauliza nikulipeni bei gani? wakaniambia tulipe dola elfu saba mia tano na thelathini na nne, na mara ya kwanza tulilipa dola elfu sita miambili ishirini…”
Bado haijafahamika kama Shirika hilo la ndege litarudisha hela ambayo ililipwa na watu hao kwa ajili ya kumsafirisha ndugu yao.

WABUNGE WACHARUKA KASHFA AKAUNTI YA TEGETA-ESCROW

Hawa ndio wabunge waliofunguka wakitaka sakata hilo lijadiliwe bungeni
Naibu spika wa bunge Job Dungai, yeye ndiye kashikilia rungu, Ripoti " ijadiliwe au la"
Mbunge wa Kigoma Kaskazini (CHADEMA), Ambaye pia ni mwenyekiti wa kamati ya bunge ya hesabu za serikali, (PAC), Zitto Kabwe. Taarifa ya CAG kuhusu akaunti nya Tegeta Escrow, iko mikononi mwake
Mnadhimu mkuu wa kambi ya upinzani bungeni, Tundu Lissu, (CHADEMA),akizunghumza bungeni mjini Dodoma jana, wakati lile sakata la IPTL, linalogubigwa na akauti iliyojichukulia umaarufu TEGETA ESCROW, lilipoibuka bungen i wakati wa kipindi cha maswali ya papo kwa hapo kwa waziri mkuu. Wabunge wanataka "ngoma" ijadiliwe bungeni, licha ya kashfa hiyo kuwa tayari mahakama kuu ya Tanzania
Mbunge wa Kigoma Kusini, (NCCR-Mageuzi), David Kafulila, huyu ndiye aliyeibua kashfa ya akaunti ya Tegeta-Escrow
Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki na mbunge wa Urambo, (CCM), Samwel Sitta
Mbunge wa Iringa mjini, (CHADEMA), Mchungaji Peter Msigwa
Mbunge wa kuteuliwa na Rais, ambaye pia ni Mwenyekiti wa NCCR-M,ageuzi, James Mbatia
Mbunge kijana, Esther Bulaya, (CCM)
Mbunge wa Longido,(CCM), Lekule Laizer,
Mbunge wa Kasulu mjini (NCCR-Mageuzi), Moses Machali, ndiye aliyemchokoza Waziri mkuu kuhusu ripoti hiyo kujadiliwa bungeni
Waziri Mkuu Mizengo Pinda, "Punguzeni jazba", akiwasihi wabunge kuwa serikali iko makini na inasubiri kwa hamu taarifa hiyo ili kila mtu hata yeye akibainika abebe msalaba wake, lakini akatahadharisha kuhusu umuhimu wa kuheshimu mihimili ya dola ikiwemo mahakama
Mbunge wa Kahama (CCM), James Lembeli

LORI LALIPUKA ENEO LA MIKUMI MKOANI MOROGORO


 Tumepokea picha ya tukio la ajali ya Lori lililokuwa limebeba mapipa ya lami ambalo limeshika moto mapema leo asubuhi maeneo ya Mikumi, Morogoro.chanzo cha mlipuko huo bado hakijafahamika mpaka sasa na bado hatujapata taarifa kama kuna aliepoteza maisha au kupatwa kwa majeruhi.Chini ni ujumbe kutoka kwa mdau wetu  alietuletea taswira hizi kuhusiana na hali ya barabara hiyo.
''Kama una safari ya kwenda Iringa-Mbeya au kama unapokwenda utapita mikumi basi sitisha safari kwani njia inefungwa tangu saa mbili asubuhi. Kuna lory linawaka moto mpaka sasa. Lilikuwa limebeba lami so lami bado inawaka na inesambaa sehemu kubwa''
Baadhi ya watu wakishudia tukio hilo la ajali.

Thursday, November 20, 2014

IPTL NI MWIBA KWA CCM


IPTL mwiba CCM
KUNA kila dalili za Baraza la Mawaziri la Serikali ya Rais Jakaya Kikwete kuvunjika tena baada ya ripoti ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kuhusu kashfa ya uchotwaji fedha zaidi ya sh. bilioni 200, kwenye akaunti ya Tegeta Escrow zilizohifadhiwa katika Benki Kuu ya Tanzania (BoT), kubainisha kuwa fedha hizo zilitolewa kinyume na taratibu.

Kashfa hii nzito ni mfululizo wa nyingi zilizotokea chini ya utawala wa Rais Kikwete na hivyo kusababisha mawaziri kadhaa kuachia ngazi akiwemo aliyekuwa Waziri wake Mkuu, Edward Lowassa aliyejiuzulu Februari 7, mwaka 2008, kufuatia kashfa ya zabuni tata kwa kampuni hewa ya kufua umeme ya Richmond.
Vigogo wa serikali wanaotajwa kuhusika katika kashfa hii ni Waziri wa Nishati na Madini, Prof. Sospiter Muhongo na Katibu Mkuu wake, Eliakim Maswi, Waziri wa Fedha Saada Mkuya, Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania, Prof.Beno Ndullu, Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Jaji Frederick Werema na Mkurugenzi Mkuu wa Tanesco, Mhandisi Felchesmi Mramba.
Wadadisi wa kisiasa wanabashiri kwamba kashfa hii huenda ikiwa mwiba wa kuking’oa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wakati huu wa kuelekea uchaguzi mkuu wa 2015, ikiwa vyama vinavyounda kundi la Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), vitadumu katika muungano wao na kuwaeleimisha wananchi madhara ya ufisadi huo.
Kashfa kama hii iliwahi kuking’oa chama tawala cha KANU cha nchini Kenya mwaka 2002, ambapo kwa mujibu wa taarifa zilizopo, mmiliki wa Kampuni ya PAP inayodai kuinunua Kampuni ya IPTL, Habinder Singh Sethi, anatajwa kuhusika katika kashfa kubwa ya ufisadi nchini Kenya ya Goldenberg, uliogharimu takribani dola milioni 600.
Ufisadi huo pia ulihusisha mahakama, watendaji, viongozi na wanasiasa wakubwa nchini humo, ikiwemo familia ya aliyekuwa Rais wa wakati huo, Daniel Arap Moi, ambapo katika uchaguzi mkuu wa 2002, vyama vya upinzani kupitia muungano wao wa National Alliance of Rainbow Coalition (NARC) chini ya mgombea wake Mwai Kibaki, kwa kutumia kashfa hiyo, vilifanikiwa kuking’oa Chama tawala cha KANU.
Kwa mujibu wa ripoti ya CAG ambayo imekabidhiwa kwa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) kwa ajili ya kuipitia na kuwahoji watuhumiwa, fedha za Escrow sh. bilioni 306 ni matokeo ya Shirika la Umeme nchini (Tanesco) kulipishwa capacity charge zaidi ya kiwango kinachotakiwa kulipwa.
Ripoti hiyo, inasema kwamba Tanesco walipaswa kurejeshewa sh. bilioni 321 zilizolipwa zaidi kwa IPTL kati ya mwaka 2002 hadi 2012. Kwa maana hiyo, Escrow ni fedha za umma. Hii ni kinyume na kauli zilizokuwa zikitolewa na viongozi mbalimbali wa serikali ya Rais Kikwete wakiwemo Waziri Mkuu, Mwanasheria Mkuu wa Serikali na Waziri wa Nishati na Madini kwamba fedha hizo ni za mmiliki wa Kampuni ya IPTL.
Kwa mara kadhaa, Waziri Muhongo amenukuriwa na vyombo vya habari akitamba na kuwabeza wabunge waliosimama kidete kuhakikisha fedha za Escrow zinarejeshwa, akidai kwamba ushahidi waliowasilisha bungeni kwa Spika wa Bunge, Anne Makinda kuonesha kwamba fedha hizo ni za umma, ni vipeperushi feki kwani yeye anao ushahidi wa makaratasi ya kujaza gari zima la tani moja kuthibitisha kuwa fedha hizo sio za umma.
Waziri Muhongo na Katibu wake, Maswi wamekuwa wakiwatuhumu wabunge David Kafulila wa Kigoma Kusini (NCCR-Mageuzi) na Zitto Kabwe wa Kigoma Kaskazini (CHADEMA) kwamba wamehongwa na aliyekuwa Mwanasheria wa Tanesco, Nimrod Mkono kushupalia sakata hilo ili kukwamisha bajeti ya wizara hiyo ya 2014/2015.
Kashfa ya Escrow imeghubikwa na utata ambapo Harbinder Sing Sethi, anadai alinunua asilimia 70 ya hisa za Mechmar kwa kiasi cha sh. milioni 500 ($300,000) ndani ya wiki tatu tu tangu hisa hizo kuuzwa kwa kampuni moja ya Visiwa vya Uingereza vya Virgin kwa sh. milioni sita.
Lakini barua ya TRA Mkoa wa Ilala, iliyosainiwa na Meneja, Paschal Kabunduguru, yenye kumbukumbu nambari TRA/DR/ILA/RE/175 ya tarehe 15/11/2013, inaonyesha kuwa kampuni ya Mechmar ya Malaysia iliuza hisa zake asilimia 70 katika kampuni ya IPTL kwa kampuni ya Piper Links investment limited mnamo tarehe 9/9/2013 kwa thamani ya sh. 6,000,000 (milioni sita).
Nyaraka za malipo ya kodi kwa mujibu wa barua hiyo inaonyesha Mechmar walilipa kodi ya ongezeko la mtaji sh. 596,000 na kodi ya stempu ya sh. 180,000 mnamo tarehe 6 Disemba 2013 katika Benki ya CRDB Tawi la Waterfront.
Katika hali inayotia mashaka, kampuni ya Piper Links nayo, kwa mujibu wa nyaraka toka TRA, ikauza hisa zake kwa Kampuni ya Pan Africa Power Solutions mnamo tarehe 30 Oktoba, 2013, takribani wiki tatu tangu kununuliwa kwa hisa hizo toka kwa Mechmar.
Kwa mujibu wa barua ya TRA, kodi iliyolipwa ni ya ongezeko la mtaji sh. 47,940,000 na ushuru wa stempu sh. 4,800,000.
Malipo ya kodi hiyo yalilipwa siku ile ile ambayo Mechmar walilipa yaani Disemba 6, 2013, jambo linalozidi kuzua utata mkubwa kuhusu mhamala huo.
Pengine kinachotia shaka zaidi ni kwamba nyaraka zote mbili toka TRA ziliandikwa siku moja, na zote zina kumbukumbu namba zinazofanana licha ya ukweli kwamba zilikuwa zinakwenda kwa makampuni mawili tofauti, moja ikiwa Malayasia, na nyingine ikiwa visiwa vya Uingereza vya Virgin.
Pia nyaraka hizi toka TRA, zinapingana na kauli ya Sethi ambaye amenukuliwa na vyombo kadhaa vya habari akidai kwamba alinunua hisa asilimia sabini za Mechmar mwaka 2010, toka kampuni ya Piper Link—mwaka mmoja kabla ya PAP kuanzishwa.
Wachambuzi wa masuala ya kiuchumi wanasema kwa mujibu wa Sheria ya kodi ya Mapato ya mwaka 2004 kama ilivyofanyiwa marekebisho katika Sheria ya Fedha ya mwaka 2012, mauzo yeyote ya hisa au mali ambazo zipo Tanzania mauzo yake lazima yathibitishwe na Wizara husika baada ya kodi zote kulipwa.
Nyaraka hizi zinaonesha kuwa mauzo ya IPTL kutoka Mechmar kwenda PiperLink na kutoka PiperLink kwenda PAP yote yamelipiwa kodi siku moja tena baada ya malipo ya fedha za Escrow kwenda PAP Disemba 5, 2013.
Kwa kuzingatia nyaraka hizo, ni dhahiri kuwa mpaka kampuni ya PAP ilipokuwa inalipwa fedha za Escrow hawakuwa na umiliki wa hisa za IPTL. Hata amri ya mahakama ilipotolewa kuwa PAP wapewe mali za IPTL, kampuni hiyo haikuwa na umiliki wa wowote wa IPTL.
Pia katika hati za kuhamisha hisa ambazo ziliidhinishwa na TRA mkoa wa Ilala, mwandiko ulipo unafanana sana na mwandiko wa nyaraka za malipo ya kodi, CRDB, tawi la Water Front—jambo linaloonyesha kwamba mtu mmoja huyo huyo ndiye aliyeandika nyaraka zote hizi.
Utata mwingine ni kuwa iweje kampuni ya VIP Engineering iliyokuwa na hisa asilimia 30 katika IPTL ilipwe dola za Kimarekani milioni 75 wakati Mechmar iuze asilimia 70 kwa sh. milioni 6 tu na PiperLink iuze kwa dola laki tatu tu ndani ya wiki tatu.
Serikali kupitia kwa Mwanasheria Mkuu wake, Jaji Fredrick Werema, Waziri wa Nishati na Madini, Prof. Sospeter Muhongo na Katibu Mkuu wake, Eliachim Maswi, wamekuwa wakisisitiza kwamba fedha hizo zilitolewa kwa kuzingatia hukumu ya MahakamaKuu.
Hukumu hiyo ya Jaji John Utamwa inapingwa na Kafulila na wadau wengine kuwa imetafsiriwa visivyo, kwani hakuna popote alipotaja Akaunti ya Escrow, ingawa katika muhtasari wa kikao kati ya Tanesco, IPTL na Wizara ya Nishati na Madini, ndipo wametafsiri uamuzi wa mahakama wakidai kwamba fedha zote za akaunti hiyo zipewe Kampuniya PAP.
Kupitia barua kumb. No. SAB.88/417/01/5 ya Oktoba 21, 2013, Katibu Mkuu wa Nishati na Madini Maswi alimwandikia Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Prof. Benno Ndulu akimtaka aruhusu fedha hizo katika Akaunti ya Tegeta Escrow.
Hata hivyo, sehemu ya ripoti ya CAG kuhusu kashfa ya uchotwaji wa fedha hizo inathibitisha kuwa TRA walibaini kuwa msingi wa ukokotoaji wa kiwango cha kulipa kodi ya Ongezeko la Mtaji ulitokana na nyaraka zenye taarifa zisizo sahihi, jambo lililochangia kutolipwa kodi ya kiasi cha sh. 8,682, 521,100.
Utawala wa Rais Kikwete umeghubikwa na kashfa nzito za ufisadi na ukiukwaji wa haki za binadamu kwa kipindi chote cha miaka tisa, lakini mara zote kumekuwa na kigugumizi cha kuwang’oa watuhumiwa mpaka pale Bunge lilipoingilia kati.
Kashfa zilizotikisa ni ile ya ununuzi wa rada mbovu kwa gharama kubwa hadi serikali ya Uingereza ikaingilia kati kushinikiza kampuni iliyouza rada hiyo irudishe chenji kwa Tanzania, pia ipo ile ya EPA iliyoaiandama serikali mwanzoni mwa utawala wa Kikwete ambapo baadaye aliyekuwa Gavana wa BoT, Daud Balali alifariki bila kuchukuliwa hatua.
Sakata lingine ni kampuni hewa ya Richmond mwaka 2008, ambapo mbali na Lowassa, mawaziri wengine waliong’oka ni Dk. Ibrahim Msabaha na Nasir Karamagi waliopata kuwa mawaziri wa Wizara ya Nishati na baadaye Baraza la Mawaziri lilivunjwa na kuundwa upya kwa Mizengo Pinda kuteuliwa kushika wadhifa wa Waziri Mkuu ambaye naye kashfa ya Escrow huenda ikamwondoa.
Zipo pia kashfa za uchangishaji fedha kinyume cha taratibu ndani ya Wizara ya Nishati na Madini iliyomhusu aliyekuwa Katibu Mkuu wake, David Jairo na kisha uchotwaji wa fedha uliyoihusisha kampuni ya Pan African Energy zaidi ya sh. bilioni 110, tuhuma ambazo ziliwangoa Jairo na Waziri wake, William Ngeleja.
Kashfa ya Buzwagi nayo ilitikisa Bunge mwaka 2007, ambapo Zitto alimtuhumu Waziri wa Nishati na Madini, Karamagi kuwa alikiuka utaratibu kwa kusaini mkataba mbovu wa mgodi huo ikiwa hotelini nje ya nchi. Hata hivyo CCM kwa kutumia wingi wa wabunge wake bungeni ilimgeuzia Zitto kibao na kumwadhibu kutohudhuria vikao kadhaa vya Bunge.
Pia zipo kashfa za ripoti ya CAG mwaka 2012 na ripoti ya Kamati Teule ya Bunge kuhusu utekelezaji wa oparesheni tokomeza mwaka 2013, ambapo mawaziri Dk. Cyril Chami, Dk. Hadji Mponda, Omary Nundu, Mustafa Mkulo, Ezekiel Maige, Dk. Athuman Mfutakamba, Dk. Lucy Nkya, Balozi Khamis Kagasheki, Dk. Emmanuel Nchimbi, Shamsi Vuai Nahodha na Dk. Mathayo David waling’oka kufuatia shinikizo la Bunge.
Wabunge CCM wakamia
Wakati PAC leo ikianza kumhoji Jaji Werema kuhusu kashfa hiyo, wabunge wa CCM wanatarajia kuwa na kikao maalum kwa ajili ya kujadili sakata hilo kabla halijaingia bungeni Novemba 27.
Kashfa hiyo, itabiriwa kwamba huenda ikamwangusha Waziri Mkuu, Pinda, kutokana na wabunge wanaomuunga mkono Lowassa kujipanga kulipa kisasi cha yale ya Richmond ya mwaka 2008.
Makamu Mwenyekiti wa PAC, Deo Filikunjombe alilieleza gazeti hili kuwa kamati yao imeshaanza kazi tangu jana, lakini leo itaanza kuhoji Jaji Werema ambaye ni mmoja wa watuhumiwa.
Mwingine atakayehojiwa ni Mkurugenzi wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) na itaendelea na kazi yake kwa kuwahoji watu wengine kadri itakavyoona inafaa.
Habari zaidi kuhusu kamati hiyo iyopiga kambi nje ya viwanja vya Bunge, zinasema kuwa itafanyakazi usiku na mchana na kukamilisha kazi yake ndani ya siku tatu.
Kamati hiyo inayoongozwa na Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe (CHADEMA), ilikabidhiwa ripoti hiyo juzi na Naibu Spika wa Bunge, Job Ndugai.
Mmoja wa wabunge kutoka CCM, aliliambia gazeti hili kuwa tayari wameshajulishwa kuwapo kwa kikao hicho kitakachofanyika siku yoyote wiki hii.
“Tutakuwa na kikao wiki hii, sijui wanataka kutuambia nini. Kama kuwatetea watuhumiwa itakuwa ngumu kwa sababu taarifa ya CAG inaonyesha wazi kwamba Waziri Muhongo, Katibu Mkuu, Maswi na wengine waliotajwa kuhusika, hawaponi. Sisi tutakuwa na nguvu gani kuwatetea? Alihoji.
Wabunge wengi bila kujali vyama vyao, wamepania sana mjadala huo na kulitaka Bunge litenge muda wa kutosha ili kila mchangiaji apate muda wa kutosha.
Mbunge wa Mtera, Livingstone Lusinde (CCM), jana aliomba mwongozo wa Spika kutaka Bunge litenge zaidi ya siku moja ya mjadala wa kashfa hiyo ya IPTL.
Alisema kwa jinsi hali ilivyo, inaonyesha kuwa wabunge wengi wanataka kuchangia, hivyo aliomba mwongozo wa Spika ili Bunge liongeze muda zaidi wa kuchangia.
Akijibu mwongozo huo, Ndugai alisema anachukua mawazo hayo na kuyapeleka kwenye Kamati ya Uongozi ili waweze kufanya uamuzi.
CREDIT: TANZANIA DAIMA

WAKULIMA BAGAMOYO WASIFIA MBEGU MPYA ZA MIHOGO.




Wakati tafiti mbalimbali zikiendelea kufanyika katika kituo cha utafiti cha MARI (Mikocheni Agricultural Research Institute)ili kulikomboa zao la Mhogo kutoka katika janga la magonjwa yaliyolikumba zao hilo,  wakulima wamendelea kusifia mbegu mpya ambazo zinaendelea kutolewa na kituo hicho kwa sasa
 Sambamba na hilo, wakulima wa mihogo wilayani Bagamoyo mkoani Pwani wamesifia ubora wa  mbegu mpya ya mihogo itokayo MARI kuwa ni mbegu bora, ikomaayo haraka, isiyo na magonjwa na pia inazaa sana tofauti na mbegu za zamani.
Wakiongea na mwandishi kwa nyakati tofauti walisema mbegu walizokuwa wakizilima hapo awali zilikuwa ni pamoja na Jota ambayo ilikuwa inakuwa ni ndefu  na inalewesha sana ukila kwa wingi, Mzungu, yenyewe ni nyekundu kwa muonekano ambayo pia hulewesha, mbegu ya Kiruthungu na Kinyafu ambazo zenyewe ni michungu sana iliwapo. Pia walisema mbegu hizi zilikuwa zinachukua mda wa miezi minne hadi mitano kukomaa kitu ambacho ni tofauti na mbegu ya sasa.
 
Walisema kuwa mbegu za sasa wamezipa majina ya Mwanamtwa, Mzuri kuonja, Kibangameno, Magimbi na kilokote, huku wakizingatia radha na uzuri wa mbegu hiyo.
Wakitofautisha mbegu mpya  walisema mbeguu mpya zote si chungu kwa kula, hukomaa ndani ya miezi mitatu mpaka mine na huzaa mihogo mikubwa kitu ambacho ni tofauti na za zamani.
“Mihogo ya siku hizi ni mitamu hata kwa kutafuna ikiwa mibichi tofauti na ile mingine ni michungu, na pia ukiipika inaunga sana mpaka inavutia wakati wa kula” alisema Ibrahim Ramadhani
Hata hivyo wananchi hao wameiomba serikali kuanzisha vipindi na majarida yanayotoa elimu ya kilimo katika vituo vya redio mbalimbali na magazeti kwani bila elimu watu wengi hufanya  tofauti na baadae kulaumu kilimo pale wanapopata hasara shambani.
“Serikali inatakiwa kurudisha vipindi vya kilimo kwani wameziacha redio zinapiga mziki asubuhi hadi asubuhi hakuna faida badala yake vijana wanaacha kufanya kazi na kukaa vijiweni kusikiliza miziki. Inatakiwa wawaambie wenye vituo vya redio kuwa na vipindi vya kilimo ili kuwabadirisha vijana wanaosubiri ajira maofisini wajue kuwa hata kilimo ni ofisi kama ofisi zingine” alisema mzee Frank Shaban.
Wakati huo huo mwandishi aliwasihi wakulima hoa kutunza mbegu hizo kwani mbegu walizopewa ni mbegu zisizokuwa na magonjwa hivyo wanatakiwa kutunza vizuri ili kupata mazao mazuri na bora kwa manufaa zaidi.
Ikumbukwe kuwa zao la muhogo lilikumbwa na magonjwa ya mnyauko fuzari pamoja na batobato ambayo yalisababisha zao hili kuwa hatarini kutoweka kitu ambacho kiliwafanya watafiti kuingia maabala na kutafuta ufumbuzi ili kukomboa mikoa inayotegemea zao la mihogo kwa chakula.
Mpaka sasa njia pekee inayotumika kuzalisha mihogo isiyokuwa na magonjwa ni tissueculturee (uzalishaji wa chupa) na njia hii haiufanyi mmea kuwa kinzani na magonjwa hivyo njia pekee ya kufanya mbegu mpya kudumu na kuzaa vizuri ni mkulima kutunza vizuri shamba lake ili kupata faida.