Tuesday, October 14, 2014

KIJANA AKUTWA AMEFARIKI KORONGONI MKOANI KIGOMA



Mwili ukiwa bado eneo la tukio 
Katika hali ya kustajaabisha kijana mmoja aliyetambulika kwa jina moja la Yusuph (Me) mkazi wa Buzebazeba Ujiji amekutwa amekufa katika korongo la Lebengera jirani na Ofisi za CCM mkoa katika manispaa ya Kigoma Ujiji huku akiwa amejaa damu katika paji lake la uso
Mara baada ya Jeshi la Polis kufika eneo la tukio walimpekua marehemu na kumkuta na fedha taslimu kama elfu tatu hivi na karatasi ambayo haikujulikana mara moja imeandikwa nini 
tukio hilo limetokea jana Oktoba13 eneo tajwa hapo juu huku umati mkubwa ukiwa umefurika ili kumtambua na kushuhudia tukio hilo, katika uchunguzi wa awali inasemekana tukio hilo limetokea jana usiku kwani kutwa nzima ya jana hapakuonekana mtu ambae amekufa eneo,akiongea na kibonajoro.com mmoja wa wananchi aliekuja kushuhudia tukio,na ambae ni mfanyakazi katika ofc moja jirani na eneo la tukio jina (....) amesema hii imekuwa ni mara ya pili kutokea tukio kama hili la mtu kukutwa ameuwawa na kutupwa katika korongo hili,hivyo tunaviomba vyombo vya usalama kuweka doria ya mara kwa mara eneo hili kwani eneo hili linakaribiana na Bar pamoja na Ofisi za Hazina Ndogo. 
Polisi wakichukua vielelezo katika picha 
Kutokana na eneo alilokutwa marehemu kuwa na miundombinu mibovu ya kumtoa walilazimika kutumia ngazi,hivyo waliomba msaaada wa ngazi kwa gali la emegency la Tanesco na hapa ngazi ilikuwa inashushwa tayari mwili kupandishwa juu kupelekwa eneo husika, 
Mwili ukitolewa tayari kupelekwa kwenye gari la Polisi 
Mwili ukiingizwa kwenye gali la Polis kuelekea Central Polis kwa taratibu zingine 
Mwili wa kijana Yusuph ukiwa ndani ya gari la Polisi,katika taarifa zingine zilizopotikana eneo la tukio zinasema kabla ya kugundulika kwa tukio hili kumetokea tukio lingine linalofanana na hili maeneo ya mwasenga usiku wa kuamkia leo mtu kukutwa ametupwa huku akiwa amepoteza maisha. 
Polisi wakiondoka eneo la tukio 
kwambali ndio eneo la ofisi za CCM mkoa ambapo kulia ndiko kumetokea tukio hili.

WAZIRI LAZARO NYALANDU AZUNGUMZIA TETESI ZA KUTANUA NA AUNT EZEKIEL NCHINI MAREKANI


Baada ya vyombo vya habari kuripoti kuhusu Waziri wa Maliasili na Utalii Lazaro Nyalandu(Pichani juu) na msanii wa filamu Aunty Ezekiel kuvinjari nchini Marekani hatimaye waziri huyo a
Aunt Ezekiel
 alisema tuhuma hizo zimetengenezwa na kundi la watu ambalo miongoni mwao ni baadhi ya viongozi wa Serikali ambao humchafua kutokana na utendaji kazi wake.

PROFESA MAZRUI AFARIKI DUNIA


 

Profesa Ali Mazrui enzi za uhai wake.
MSOMI mashuhuri wa masuala ya kisiasa, utamaduni wa Kiafrika na dini ya kiisilamu wa nchini Kenya, Profesa Ali Mazrui ameaga dunia leo akiwa Marekani.
Mazrui alyekuwa anaishi nchini Marekani, amefariki akiwa na umri wa miaka 81baada ya kuugua kwa muda mrefu.
Taarifa zinadai kuwa Profesa Mazrui atazikwa mjini Mombasa, Pwani ya Kenya alikozaliwa.
Enzi za uhai wake, marehemu alitoa ombi la kutaka kuzikwa Mombasa akisema angependa kuzikwa katika jumba la kihistoria la Fort Jesus.
Kabla ya kifo chake, Marehemu Mazrui alikuwa anafundisha katika Chuo Kikuu cha Binghamton mjini New York, Marekani.

PAPAA MSOFE NA MAKONGORO WAENDELEA KUSOTA RUMANDE


Papaa Msofe (katikati) akishuka ngazi za Mahakama ya Kisutu. (Picha na maktaba yetu).
MFANYABIASHARA anayekabiliwa na kesi ya mauaji, Marijan Abubakar, maarufu kama Papa Msofe na mwenzake, Makongoro Joseph, wameendelea kusota rumande kutokana na kile kinachoelezwa kuwa upelelezi bado haujakamilika. 
Kesi ya watuhumiwa hao wawili imetajwa leo na mwendesha mashitaka wa serikali, Bi Hellen Moshi katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam mbele ya Hakimu Mkazi, Hellen Liwa.
Msofe na Makongoro wanakabiliwa na kesi ya mauaji ya bwana Onesphory Kitoli.
Kesi hiyo imeahirishwa mpaka Oktaba 27, mwaka huu itakapotajwa tena.

KILIMO BORA CHA MANANASI KIMEBADIRI MAISHA YA WANAWAKE WA KIWANGWA NA FUKAYOSI WILAYANI BAGAMOYO.



Japokuwa kumekuwa na dhana ya kwamba mkulima ni mtu maskini na asiyeweza kufanya shughuli nyingine ya maendeleo, lakini kwao UFUMAKIFU wanajiuliza walikuwa wapi kufanya kilimo hiki tangu siku nyingi.
Akiongea na mwandishi wa habari Bi Farida Mrisho Pyara, mwenyekiti wa kikundi cha UFUMAKIFU (Umoja wa wanawake Kiwangwa na Fukayosi) alisema kuwa kilimo cha mananasi kimekuwa mkombozi kwao kwani tangu walipoanza kujishughulisha na kilimo hicho kama kikudi maisha ya wanakikundi wengi yamebadirika kutoka katika hali duni na kuwa bora zaidi.
Kikundi hicho kilianzishwa mwaka 2012 na shirika la DotAfrika kwa madhumuni ya kuwakwamua wanawake kimaendeleo katika kazi zao, kina wanawake zaidi ya 50 wa umri tofauti tofauti. Walianza kwa kuwa na shamba la pamoja ambalo walilima wanachama wote kwa kupanda mbegu mpya kutoka chuo cha SUA ambazo walipewa na shirika hilo kama msaada.

Hata hivyo mwenyekiti huyo alidai kuwa baada ya kulima kama kikundi lakini lilikuwa ni darasa tosha kwao kwani walijifunza mambo mengi mapya ya jinsi ya kulima kilimo bora  na kutumia mbegu bora za mananasi kwa kupata mavuno bora kwa manufaa zaidi.

 Bi farida alisema shamba hilo ambalo lilikuwa kama ni shamba darasa kwao liliwapa mafunzo ambayo kwa sasa kila mwanakikundi ana shamba lake na analima kwa kutumia ujuzi uleule walioupata hapo awali na kila mmoja amefunguka na kutambua kuwa walikuwa wanadharau kilimo kwa kuwa walikosa elimu ya kutosha, ni jinsi gani wanaweza kufanya kilimo chenye manufaa kwao.
“Wanawake wengi tulikuwa tunafanya biashara ndogo ndogo huku tukiwaachia wanaume kwenda mashambani peke yao, matokeo yake wengi wetu tulibaki kuwa tegemezi na inakuwa hali mbaya zaidi ikitokea mwanaume kafariki. Lakini tangu tumeanza kikundi hiki wengi wetu tuna mashamba yetu binafsi ambayo hutupatia kipato cha kutosha” alisema Bi Farida. 
Hata hivyo alisema mpaka sasa kila mwanachama anashamba lake ambalo analilima mwenyewe kama shamba darasa, na iwapo wanapata  tatizo linalohitaji ufumbuzi wanae Afisa kilimo Bwana Amir Abdul ambaye amekuwa msaada mkubwa sana kwao kwani ndiye anayewapa elimu ya kilimo kila wanapohitaji elimu hiyo.



Nae Bi Halima Muhamed Athumani (58) mjumbe wa UFUMAKIFU alisema elimu waliyopewa ni bora na isiyo ya gharama katika kufanikisha kilimo hicho.
“Tumeletewa mbegu za mananasi isiyokuwa na magonjwa yaliyokuwa yanatusumbua kipindi cha nyumaa, na tumejifunza njia ya kulima bila kulichosha shamba wakati huo huo tunazuia matunda yasiharibiwe na jua kwa kupanda mazao mawili shambani yaani mananasi na migomba pamoja, wakati huo huo tunarutubisha shamba kwa kuchoma masalia ya nanasi shambani baada ya kuvuna kitu ambacho  tulikuwa hatukijui hapo awali”. Alisema Bi Halima
“Siku hizi huwa tunaweka mbolea ya DAP na UREA kwa ajili ya kukuzia na hatutumii dawa ya aina yoyote kuzuia magonjwa kwani mbegu hii haina usumbufu huo. Na pia mbegu hii inawahi kukomaa.”
Aliendelea kwa kusema mbegu hii ni nzuri kwa kuwa hainyauki tunda wala kuozea shambani na inatoa mazalia bora pia ambayo huwa yanakuwa ni mbeyu kwa ajili ya kupatwa msimu mwingine nah ii ni tofauti na mbegu tulizokuwa nazo siku za nyuma

 Kikundi hicho ambacho kwa sasa kimeamua kulima kilimo cha kisasa kwa ajili ya kuondoa umaskini majumbani mwao, wameamua kwenda mbali zaidi kwa kufanya biashara ya mananasi nje ya nchi na mikoa ya mbali kwa kuyasindika mananasi na kuyasafirisha.
“Hivi saasa tumejenga makaushio (dryer) kwa ajili ya kukausha mananasi na kuyahifadhi vizuri kwenye mifuko tayari kwa kuyapeleka sokoni ili kuwa na tija zaidi. alisema Mwenyekiti huyo

Bi Farida akiwa ndani ya makaushio (dryer) akitoa maelezo jinsi kipima joto kinavyofanya kazi

Kilimo cha nanasi kinastawi zaidi katika ukanda wa nchi za joto na kwenye udongo usituamisha maji. Hapa Tanzania zao hili linastawi sehemu nyingi lakini kwa wingi linastawi mikoa ya Pwani, Morogoro, Shinyanga Tanga Mtwara Lindi na Bukoba. Katika mkoa wa pwani, zao hili linalimwa katika wilaya ya Bagamoyo, Mkuranga Kibaha na Kisarawe. Kwa Bagamoyo linalimwa zaidi katika kata ya Kiwangwa na maeneo ya Gongo.
Zao hili lina kiasi kikubwa cha vitamini A na B na kiasi kidogo cha vitamini C, pia kuna madini kama potasiam, kalsiam, chuma na magnesiam
Nanasi huliwa baada ya kumenywa ganda la nje na pia hukamuliwa maji yake na kunywa kama juisi.Nanasi pia linaweza  kuanikwa na kukaushwa ambapo huliwa kwa kutafunwa. Nanasi pia baada ya kukauka husagwa na unga wake hutumika kutengeneza juisi au kuchanganywa katika vilaji vingine kama vile Pizza nk


Monday, October 13, 2014

BIBI NA BWANA HARUSI WANUSURIKA KIFO

bibi harusiBibi harusi Mariamu mduwa aliyenusurika kifo katika ajali ya mitumbwi katika kijiji cha kalalangabo akiwa naendelea na matibabu katika hospital ya  mkoa wa Kigoma

 
 
 
wawili hawa wamenusurika katika ajali ya mtumbwi iliyogharimu vifo vya watua zaidi ya 10 baada ya boti waliyokuwa wakisafiria kuzama ziwa Tanganyika
Akiongea na mtandao huu katika wodu namba 5 katika Hospital ya Mkoa wa Kigoma alipolazwa bibi harusi huyo alisema kuwa alishikwa na bumbuwazi sana baada ya tukio hilo kwani mpaka sasa bado hajielewi.
”Sikumbuki kitu kwani baada ya mtumbwi kuzama kila mtu alikuwa anahangaika kujiokoa na kifo,kwakweli mimi naona kama mkosi siku ya harusi yangu watu wanakufa ila namshukuru mungu kwa kutunusuru na kifo na yote mimi nimemwachia mungu”alisema bibi harusi huyo
Muhanga mwingine aliyenusurika katika ajali hiyo Zabibu Issa alisema kuwa mitumbwi waliyokuwa wamepanda ilikuwa imejaza sana watu na mizigo ndiyo maana ilizidiwa uzito na kuzama baada ya kupigwa na wimbi.
”Safari ya kwenda kijijini kwetu lazima tupite njia za majini hakuna barabra kabisa sababu vijiji tunavyoishi vipo mwambao mwa ziwa Tanganyika kungekuwa na barabara tungepita barabrani”alisema Mhanga huyo
 


wahangaNdugu jamaa na wapambe wa bwana na bibi harusi walionusurika kifo baada ya ajali ya mtumbwi kutokea katika kijiji cha kalalangabo wakiwa wanaendelea na matibabu katika hospita ya Mkoa wa Kigoma
bibi harusi
 
Naye muuguzi wa wodi namba tano walipolazwa majeruhi hao alisema kuwa wamejuhi wote waliopo wodini hali zao zinaendelea vizuri na mpaka sasa wameshapokea jumla ya maiti sita.
Kamanda wa polisi wa Mkoa wa Kigoma Jafari Mohamed alisema kuwa mpaka sasa jumla ya watu 27 wameshaokolewa,na miili sita kuopolewa pamoja na walionusurika 11,lakini bado inahofiwa kuwa kuna miili mingine zaidi ambao bado haijapatikana kwani mitumbwi hiyo inakadiriwa kuwa ilikuwa na watu zaidi ya sabini.

 UOKOJIWaokoaji mbalimbali wakijindaa kwenda katika eneo ilipotokea ajali ya mitumbwi iliyobeba harusi kutoka kigoma mjini kwenda katika kijiji cha Kigalya kutafuta miili ya marehemu ambayo bado haijapatikana

KIJANA ATEMBEZWA UCHI MTAANI KWA KUTAFUTA PESA ZA KUFANYIWA TOHARA

Kijana mmoja nchini Kenya alilazimishwa kutembezwa akiwa mtupu mtaani ili kuchangisha fedha za kumuwezesha kufanyiwa tohara.
Hatua hiyo ilikuja baada ya kijana huyo kudai hana pesa ya kwenda kufanya tohara na wanaume wenzake kuamua kumtembeza mitaani ili aweze kusaidiawa kupatiwa kiasi cha pesa kitakachomwezesha kufanyiwa huduma hiyo.
Kiongozi wa kundi lililokua likimtembeza mitaani  Peter Mwogera alisema lengo la kumzungusha mitaani uchi ni kutaka jamii ya watu wa Githurai waamini kuwa kijana huyo alikua hajafanyiwa tohara.