Tuesday, August 5, 2014

MCHUNGAJI GWAJIMA ANUNUA KELKOPTA KWA AJILI YA KUHUBILI IJILI


Habari ambazo zimethibitishwa na facebook page ya kanisa la Ufufuo na Uzima zinasema kuwa Helkopta hiyo imewasili nchini tayari na sasa inafanyiwa assembling kwaajili ya kuanza kuruka jumatatu hii. Tukio ambalo limelifanya kanisa hilo kuandaa ibada maalumu ya kumshukuru Mungu kwa kupokea helcopta hiyo itakayotumika kusambaza injili Tanzania.

http://api.ning.com/files/8QOPGYNO0th3hDpF3ZzAN6rfTh*W*jBrdgEoTYC0my1gOuhr1-Lx1*zIWR9nYs5jhHgYVwky3pRkLrtzGyAhnPH1bJZRRjQP/3.JPG Helcopta hiyo aina ya R44 ni mali ya kanisa la Glory of Christ T Church ambalo liko chini ya mch. Gwajima. Akiongea Jumapili iliyopita kanisani kwake Kawe Mch. Gwajima alisema huku akimsimamisha Mjapani mmoja ambaye kwa mujibu wa Mch huyo ndiye aliyefanikisha ununuzi wa helkopta hiyo ya kwanza nchini kutumika katika kusambaza injili.

http://api.ning.com/files/8QOPGYNO0tiUr8eYWK9Fm933U6QmLMwodxNtvp9FP-NNCrld48tPWB*ms1P3N2nchFGBo4UdflCTj82xU7Vzl3WYuKdJT0KI/8.JPG Aidha, Mchungaji Gwajima alitumia muda huo kutoa Ufafanuzi juu ya kuwepo kwa taarifa za yeye kushirikiana na Nabii maarufu GeorDavie kuzindua helcopta hiyo alisema, "Nabii GeorDavie amepanga kukodi helcopta aina sawa na yetu (R44) na atatua nayo kwenye kanisa lake (ambalo pia lipo maeneo ya Tanganyika Packers) akitokea Arusha. lakini mjue wote kuwa helkopta hiyo si ambayo kanisa la Ufufuo na Uzima imeinunua bali imekodiwa seacliff na wala hatujaandaa mkutano wa pamoja na Nabii huyo" mwisho wa kunukuu.

Hii inakuwa Helkopta ya kwanza kutumika kuhubiri injili ikiwa ni mali ya kanisa. Ibada ya shukrani kanisani Ufufuo na Uzima ilihudhuriwa na waimbaji kama Munishi akiwa na  Malebo (ameokoka), Rose Muhando, Bony mwaitege, John Lisu, Upendo Nkone, Flora Mbasha, Christina Shusho na wengine wengi..

na hivi ndivyo ilivyokuwa katika picha

 





http://api.ning.com/files/8QOPGYNO0thVD5Z2ZXMhFUd2-tjN-msoo1bW0pt2yGE-kYmD*13httGa-v9*TAdF5wFjat1sfQFqNhD24QHx6nPxPebcvnTw/5.JPGhttp://api.ning.com/files/8QOPGYNO0thAIrHwtmiffKtvs56VYEH*5kchDhsDlQI3EeohoBmpIY7JdeRz-wJSqdCOe8QSTnTN-jRcb2EGyPPkDYUYRqvt/6.JPG

No comments:

Post a Comment