Wednesday, September 3, 2014

LUKUVI AZOMEWA MBELE YA RAIS KIKWETE


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge), William Lukuvi amejikuta katika wakati mgumu mbele ya Rais Jakaya Kikwete baada ya kuzomewa hadi kukatisha hotuba yake akipingwa na wananchi pamoja na madiwani wa CCM wa Halmashauri ya Manispaa ya Dodoma alipokuwa akitetea kuwapo kwa Mamlaka ya Ustawishaji Makao Makuu (CDA).

Lukuvi alikumbana na mkasa huo wakati akijibu hoja za Mbunge wa Dodoma Mjini (CCM), David Malole ambaye alitaka CDA ivunjwe akiituhumu kuwavunjia wananchi nyumba bila kuwatafutia mahali pa kuishi.

Hoja ya Malole kutaka CDA ivunjwe iliibuka katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika Kata ya Kikuyu, Manispaa ya Dodoma baada ya Rais Kikwete kuzindua ujenzi wa Barabara ya Dodoma - Iringa.

No comments:

Post a Comment