Mwanamke
wa Mexicana, Leandra Becerra mwenye umri wa miaka 127 anaetajwa kuwa mtu
mwenye umri mkubwa zaidi duniani ameeleza siri ya kuishi miaka mingi
zaidi.
Kwa
mujibu wa mjukuu wake mwenye umri wa miaka 45, bibi huyo alimueleza kuwa
siri ya ‘yeye’ kuishi miaka mingi ni kula vizuri, kulala kwa muda mrefu
na kuishi bila kuolewa. Bi
Leandra ambaye alizaliwa August 31, 1887 alikuwa mpiganaji wakati wa
mapinduzi ya Mexico mwaka 1910-1919 na alikuwa kiongozi wa kundi la
‘Adelitas’ ambalo lilikuwa linaundwa na wanawake wanaoenda vitani na
waume zao.
Bibi huyo ambaye ana wajukuu wengi huku mjukuu wake mkubwa akiwa na umri wa miaka 73, tayari ameshawazika watoto wake watano.
Mjukuu wake aliiambia gazeti la El Hozizonte la Mexico kuwa bibi huyo hivi sasa anatatizo la kubwa la kusikia.
Ameeleza
kuwa bibi huyo mara nyingine hulala mfululizo kwa muda wa siku tatu huku
akipewa chakula pale anaposhituka. Lakini akiamka hupenda kula mlo
kamili kwa uhakika, kuimba, kutaniana na kusimulia hadithi mbalimbali
zinazohusu maisha na mapambano ya mapinduzi ya Mexico.
CHANZO:BONGO5
No comments:
Post a Comment